Takwimu hizo za kipindi cha miongo miwili kutoka Idara ya Taifa ya Takwimu zinaonyesha watoto wanaozaliwa huongezeka sana wiki 40 (miezi 9) baada ya msimu wa sikukuu.
Hili huenda linatokana na wanandoa kutumia muda mwingi pamoja wakisherehekea, au kulenga makusudi mwanzo wa mwaka mpya wa shule ambao huanza mapema Septemba nchini humo.
“Ongezeko la watoto wanaozaliwa mwishoni mwa Septemba ni ishara kwamba mimba nyingi hutungwa wiki chache kabla ya Krismasi na kuendelea hadi siku chache baada ya Krismasi kuliko wakati mwingine wowote wa mwaka,” idara hiyo imesema.
Kawaida watoto 1,800 huzaliwa kila siku lakini idadi hii hupanda hadi 1,974 siku yenye kuzaliwa watoto wengi zaidi ambayo ni Septemba 26.
Siku zinazoshuhudia idadi ndogo zaidi ya watoto wanaozaliwa ni siku za Krismasi, Boxing Day na siku ya Mwaka Mpya.
Hili sana huenda linatokana na idadi ndogo ya watu wanaopangiwa kujifungua kwa kufanyiwa upasuaji siku hizo, kwani huwa ni siku za mapumziko.
Profesa wa masuala ya uzazi kutoka Chuo Kikuu cha Sheffield Allan Pacey ameambia BBC: “Wazo kwamba mimba nyingi hutungwa wakati wa Krismasi lina msingi. Nina uhakika sherehe na shamra shamra za wakati huu huchangia.”
"Nimefurahi kuona wengi wamejitokeza kunisupport kuungana nami siku ya tareh mbili kwenda nami kutembelea katika Wodi ya Kina mama na Watoto na kuwapelekea kidogo nlichojaaliwa kupitia Mauzo ya Mkito.com na TIGO kama Shukran yao kwangu..... Hii ni kwa nduguzangu wa Mitandao ilokuwa imesalia... tafadhali naomba mnisupport kwa kuifanya nyimbo ya #UTANIPENDA kama mlio wa mtu akupigiae (Callertune)... angalia kwa picha Neno na kisha tuma kwa namba iliyoambatanishwa na Mtandao wako...." #MZIIKI VODACOM tuma BF4924 kwenda 15577 AIRTEL tuma CT5234929 to15578 ZANTEL tuma SET0600035045 kwenda 15098 UNGANA NAMI INSTAGRAM @PAULCHAZZY
1. Mwanaume ambaye atamuheshimu, wanaume wengi hujiona wao kuwa ni bora zaidi ya wapenzi wao na kuwaona wapenzi wao kuwa ni kifaa cha mapenzi tu.
2. Mwanaume mwenye upendo wa dhati, unaweza kuwa na mali kama magari, majumba na visitoshe kumfanya mwanamke awe na furaha na uhusiano zaidi ya mapenzi ya dhati.
3. Mwanaume ambaye atamlinda na pia atakaye mwamini kuwa anaweza kukabiliana na shida ambazo mwanamke atakabiliana nazo sio lazima katika mali bali hata hari pia.
4. Mwanaume ambaye atajivunia kuwa nae kutokana na uhamasishaji (public figure) kwa watu wengine haijarishi katika namna gani ili mradi iwe namna ambayo itakuwa na malengo mazuri kwa jamii mfano, mfanyabiashara mkubwa, anaejiheshimu, mpambanaji n.k
5. Mwanaume mwenye shauku kwa sababu wanawake wengi huongea sana na hupenda kuongea na wanaume zao sasa usipokuwa na shauku unamkatisha tamaa.
6. Mwanaume mwaminifu na ambaye atamtegemea, haijalishi mwanamke anafanya kazi au la anahitaji uaminifu wako na msaada wako katika nyakati zote.
7. Mwanaume muungwana. Uungwana ni kitu kizuri na huvutia watu wengi na sio alama ya udhaifu kama inavyodhaniwa na watu wengi.
8. Mwanaume mwenye msimamo na mwenye kufanya maamuzi yake mwenyewe na sio mwenye kutegemea maamuzi ya familia yake au wenzake.
9. Mwanaume mwenye malengo, mwanaume ambaye huna malengo na kesho yako na huna mipango yoyote sio chaguo la mwanamke na utaishia kuwa na wapenzi tu na sio mke.
10. Mwanaume mwenye mtazamo chanya wa maisha na sio yule anayefikiria kubadilisha mitindo ya nguo na ya nywele kila kukicha pasipo kujituma.
NIFOLLOW INSTAGRAM KWA UPDATES ZAIDI @PAULCHAZZY
Mbinu mpya ya kusafirisha data ambayo hutumia mwangaza badala ya mawimbi ya radio imejaribiwa.
Li-fi ina uwezo wa kumfanya mtumiaji kupata huduma ya mtandao mara 100 zaidi ya Wi-Fi na hutoa kasi ya hadi Gigabait moja kwa kila sekunde.
Li-Fi inahitaji mwangaza kama vile wa glopu,huduma ya mtandao na sensa ya picha
Ilijaribiwa wiki hii na Velmenni mjini Tallinn Estonia.
Velminni ilitumia glopu ya li-fi inayoweza kusafirisha data kwa kasi ya Gigabait moja kwa sekunde.
Jaribio la maabara limeonyesha kuwa li-fi ina kasi ya hadi Gigabait 224 kwa sekunde.
Ilijaribiwa katika afisi ili kuwasaidia wafanyikazi kupata huduma ya mtandao na katika kiwanda ambapo iliweka mwangaza.
Prudhoe Bay, Alaska
Picha za baadhi ya vyoo vya ajabu zimeonyeshwa kudhihirisha namna dunia ilivyokuwa na hali mbaya kiusafi.
Picha hizo zinahusisha choo kimoja kilichojengwa kwa mbao katika bustani na ni cha umma kikiwa kimezungukwa na theluji mjini Alaska.
Jimbo la Yenagoa, Bayelsa nchini Nigeria’
Umoja wa Mataifa umesema watu bilioni 2.4 duniani hawatumii vyoo vizuri na wako hatarini kupata magonjwa.
Tazama picha nyingine za vyoo hivyo;
Choo cha baa mjini Paris
Choo cha nyumba mjini Lalitpur, Nepal
Choo cha umma kijijin cha Gatwekera katika makazi duni ya Kibera mjini Nairobi, Kenya
Chhattisgarh, India
Ciudad Juarez, Mexico
Abidjan, Ivory Coast
Chiba, Tokyo
Yuzhno-Kurilsk, Urusi
Choo cha wasichana Algiers, Algeria
Lima, Peru, na huwa hakuna maji katika eneo hilo
Choo cha nyumbani Mandalay, Myanmar
Choo cha umma London Fields mjini London
Choo cha baa Rio de Janeiro, Brazil
Choo cha umma mjini Istanbul, Uturuki
Choo cha nyumbani Palestina
Choo cha hoteli mjini Santa Monica, California, United States
Roma, Italia
Tibet, China
Vyoo vya umma katika mji wa Al Azraq, Jordan
Choo cha nyumgbani mjini Mexico City, Mexico
Choo cha mgahawa mjini Brooklyn, New York,
Choo mjini Illinois, Chicago
vyoo vya dharura Cape Town, Afrika Kusini
Choo cha kuhama mjini Kathmandu, Nepal
Choo cha nyumani huko Manly mjini Sydney, Australia
Tbilisi, Georgia
Huruhusiwi kukojoa mjini Hanoi, Vietnam
Choo cha nyumbani mjini Hong Kong, China
Choo cha saluni mjini Frankfurt, Germany
Beijing, China
Vyoo vikiwa sehemu ya wahamiaji haramu katika kisiwa cha Kos, Greece
Baalbek, Lebanon, vyoo hivyo vimejengwa kwa ufadhili wa Unicef
Vyoo cha hoteli ya kimataifa mjini Pyongyang, North Korea
Choo cha umma katika mtaa wa Oscar Freire mjini Sao Paulo, Brazil
Vyoo vya umma katika kijiji kilochopo Beijing, China
Vyoo vilivyopo katika kumbukumbu za piramidi mjini Cairo, Egypt
Choo mjini Munich, Ujerumani Kusini ambako wanaishi watu wanaotafuta hifadhi
Vyoo vya umma mjini Oslo, Norway
Choo kilichopo nje ya mji wa Santiago, Chile
Alamogordo, New Mexico, Marekani
Ramani ikionyesha nchi zenye vyoo vizuri duniani ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Choo Duniani
Haijalishi ni kiasi gani unayaona maisha yako kuwa ni mabaya,..usikate tamaa ,kuna watu hawana viungo vyote vya mwili kama wewe,but Mungu Kakupa,unakula milo miwili,mitatu hata mmoja kwa siku,lakini kuna mtu sehemu anatamani ale tu hata hicho unachokibakiza mezani..Usikate tamaa
siku zote amka ukiwa na moyo wa kusamehe,kushukuru kwa kila jambo na zaidi,appreciate kwa chochote Mungu anachokubaliki,Zingatia...
MAFANIKIO NI LAZIMA KWA KILA ANAEFANYA KAZI KWA BIDII NA UAMINIFU.
USIKOSE KUNIFOLLOW INSTAGRAM @PAULCHAZZY
KWA UPDATES ZAIDI.
1. Kukaa peke yako na kuanza kupiga hesabu kwa pesa ambayo hauna, utakuta kijana ametulia anaanza kupiga mahesabu nikipata milioni 10 nitafanya 1, 2, 3,……n.k. Na hii huwatokea vijana wengi sana.
2. Kupiga piga rimoti na kubonyeza wakati tunajua kuwa betri zimeisha na ikikubali hununui tena betri utazani tatizo limeisha kumbe lipo pale pale.
3. Kutoboa tube ya dawa ya meno au kopo la mafuta ili kukombeleza masalia kwa ajili ya kutumia.
4. Kusimama mbele ya kioo na kuanza kujitizama huku ukiweka mapozi mbalimbali kwa maringo. Unashtuka kuna mtu alikuwa anakuona unaanza kuzuga.
5. Kufanya usafi siku anapokuja mgeni, na hii iko hasa kwa vijana wanaoishi “getto” na pia wadada wengi huwa na nguo za ndani zilizotoboka wakidai ni za kuvaa nyumbani, sijui siku ikitokea dharura itakuwaje mi simo.
6. Kuongea na simu huku ukifanya mambo mbali mbali ya ajabu unaweza ukapewa hata moto na ukapokea au kuweka kiatu ndani ya friji yaani akili yako inakuwa haiko eneo husika kabisa.
7. Unasoma kitabu au kitu chochote lakini akili yako haipo na unakuja kushtuka uko kurasa ya tatu au ya mbele zaidi na hujaelewa chochote. Hahaah.
8. Upo katikati ya watu mara simu inaita unaangalia kama ni simu yako wakati mlio wako haufanani kabisa na mlio ulioita. Hahaah...
9. Umeongozana na mtu mnapiga stori ghafla anasimama wewe hujui unaendelea tu kuongea na mtu mwingine wala hata hakufahamu unakuja kushtuka mbali sana. Dah aibu
10. Umekutana na mtu unahisi kama unamfahamu na unaanza kumuuliza kasoma wapi ili ujue mlikutana mazingira gani masikini kumbe ulimuona kwenye TV.
NIFOLLOW INSTAGRAM KWA UPDATES ZAIDI @PAULCHAZZY
1.Wanamuziki waliokuwa wakipiga muziki kwenye meli ya titanic, waliendelea kupiga muziki kwa saa moja Toka meli ilipoanza kuzama.
2.Gharama za kutengeneza Movie ya Titanic Ni Kubwa kuliko gharama za Kutengeneza Meli halisi ya Titanic iliyokuwa na uwezo wa kubeba watu zaidi ya elfu tatu! Movie ya Titanic ilitengenezwa kwa gharama ya dola Milioni miambili ($ 200Mil) wakati Meli ya Titanic ilikuwa na thamani ya $170 Mil.
3. Baada ya Kuona Meli inazama Maeneo yenye baridi kali, Mpishi Mkuu wa meli hiyo, alikunywa pombe Kupita Kiasi ili aweze Kuhimili baridi Kali! Aliweza Kukaa masaa Mawili kwenye Barafu na Hatimae Kuokolewa.
4.Sekunde 30 zingetosha Kuokoa Meli ya Titanic Kama si Kuchelewa Kutoa Taarifa za Kuwepo kwa Mwamba wa Barafu. Watoa taarifa walichelewa kwa Sekunde 30 tu!
5.Baada ya Kugongana na Mwamba, Ilipita masaa mawili mpaka Meli yote ya Titanic Kuzama.
6.Hakuna Meli Yoyote nyingine Iliyowahi Kuzama kwa kugonga Barafu!
7.Mjapani Aliyepona kwa kuokolewa Kwenye Ajali ya Titanic, aliitwa Mpumbavu nchini kwake eti tu, Kwanini hakufa kishujaa pamoja na wengine?
8. vyumba vya Hadhi ya juu zaidi kwenye Meli ya Titanic vililipiwa Dola 200.
9. Zaidi ya Maharusi 20 walikuwa wakisherekea “HoneyMoon” kwenye meli hiyo iliyozama.
10. Msanii Madonna ni moja kati ya watu waliotakiwa kuigiza uhusika waa “Rose” lakini baadae Kate Winslet aliigiza uhusika huo