technology

business

SPORT:MOURINHO AZIDI KUAHA KUMBAKIZA DAVID LUIZ CHELSEA.

Ukitaja jina la David Luiz kwa kocha wa Chelsea Jose
Mourinho basi nadhani ni maumivu ya kichwa yanoyatawala
kichwani mwake na akili yote kuznguruka kutafuta
dawa ya kuweza kumbakiza beki huyu wa kati mwenye asili ya
kibrazil kwa wazee wa ''The Blues''

Lakini Hali inaonekana kuwa ngumu kila kukicha baada
ya timu kama Barcelona kuonesha nia ya kumsajiuli beki huyu
licha ya kuwa bado ana mkataba wa mwaka mmoja
 na klabu ya chelsea ya Uingereza...
Katika mazungumzo na waandishi wa habari akijibu
swali la mwandishi wa habari kutoonekana
kwa David mazoezini alikuwa na haya ya kusema
''Bado nazungumza na kijana wangu,napenda kumuona
akizidi kuwepo nasi hapa na yupo kwenye mikakati yangu
ya kugombea ubingwa wa vikombe vingi
nikiwa hapa darajani''

Alizidi kufunguka juu ya Kupokea Ofa toka kwa
 Barcelona alikuwa na haya ya kusema
''Unajua aikatazwi kwa timu yoyote kupendezwa
na mchezaji yoyote lakini lazima
sheria zifatwe lakini licha ya hivyo sisi kama timu
atuna mpango wa kumuuza
David kwa timu yoyote,tupo nae mezani kushugulikia
maswala yake ya mkataba mpya
na ni maswala kadhaa tu yanamaliziwa na hali itakuwa shwari'' Alisema
Kocha huyo anaejulikana kwa jina la 'The Special One'

Habari za ndani zimeweza patikanika ni kwamba
David Luiz amezidi kuwachanganya
uongozi wa Chelsea baada ya kugomea kusaini
mkataba mpya na kinachosemekana
ni kwamba anaona kama ni dharau yeye
 kucheleweshewa kupewa mkataba mpya
kilabuni hapo so aina budi yeye kuangalia njia
nyingine ya kujinufaisha zaidi.

Swala hili ndilo lazidi kumchanganya Kocha
 Jose Mourinho kwa hali zaidi.....
Tusubiri tuone kitakachojiri mwishoni mwa
dirisha la usajili litakavyofungwa
mnamo tarehe 31.8.2013....Je David Luiz atabakia
 Chelsea au Kutimkia Barcelona....?

Usikose kupitia Blogsite yako hii ya Kijanja
zaidi kupata Updates za uhakika zaidi...

Ebu otea David Luiz atachezea timu gani kabla ya dirisha la uchaguzi alijafungwa....?

SUBMIT VOTE vote to see results
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

No comments :


three columns

grids

health